Pages

Jinsi ya Kutengeneza Kachori

Mahitaji

1 pound nyama ya kusaga
5 - 6 viazi ulaya 
2 vijiko vya chakula mafuta ya kupikia
1 kijiko kidogo cha chai cumin powder
1 kijiko kidogo cha chai coriander powder
2 pilipili mbuzi
1 tangawizi
¼ kijiko cha chai garam masala
2 vijiko vya chakula maji ya limao au ndimu
 Pinch chumvi upendavyo
1 kijiko cha chai kitunguu swaumu
5 mayai ya kuku
Mafuta kwa ajili ya kukaanga

Jinsi ya Kutengeneza 
Chemsha viazi kwenye sufuria vikiwa na maganda yake.

Weka nyama ya kusaga, kitunguu swaumu na malimao na  kuikaanga mpaka maji yaishe. Halafu weka maji kidogo kidogo na kuichemsha mpaka iive. Weka pembeni.

Menya viazi ulivyochemsha kisha kata katika vipande vidogo. 

Pasha mafuta ya kupikia kijiko kimoja kwenye kikaango.

Weka cumin, coriander powder, pilipili, tangawizi halafu weka chumvi na viazi. 

Kaanga kwa dakika 2-3 itakua imeiva vizuri.

Ponda mchanganyiko wako mpaka uwe laini kabisa

Chukua mchanganyiko huo wa viazi na tengeneza maumbo madogo ya mviringo ukubwa kama limao kisha bonyeza kwa kutumia kidole kati kati ya umbo hilo utapata nafasi ya kuweka kijiko kimoja cha chai nyama ya kusaga iliyoiva kisha funika kwa kutumia viazi na jitaidi kuviringisha tena kwa kutumia mikono yako miwili ili upate umbo zuri.

Piga mayai pembeni kwenye bakuli na chovya umbo moja moja na weka kwenye kikaango chenye mafuta ya moto kaanga ukishapata rangi tu ya kahawia toa.

No comments:

Post a Comment